Thursday, November 11, 2010

RESHMAIL

Hakujua hakujua kama ipo siku mapenzi yatamtesa,lakini sasa alikuwa mtumwa.

Sunday, November 7, 2010

MAHABATI YA KIKURYA

Mwili wake uliojengeka kikamilifu,kifua kipana na urefu wake uliosindikizwa na ngozi ya maji ya kunde vilimshawish kila binti kukiri kwamba Geofrey Kazimoto alikuwa mtu wa shughuli pevu kitandani,"Umbo langu halijengwi na mpira wa miguu wala gym" alipenda kujitapa Geof kila anaposifiwa kwamba "He is gentleman" ni ukweli mtupu wala alikuwa hajisifii hata kiduchu ,Geof alikuwa mtu wa totoz kila wiki aliweza kubadili hata mara tatu,si yeye aliyewatongoza mara nying wengne walitaka huduma wenyewe hata bila neno "NAKUPENDA" kati yao,mh! sijui walikuwa wanapata nini lakin kamwe hawakuisha katka geto la Geof.
Kitanda chake ni rafiki zake pekee waliokiita sita kwa sita lakin kila bint aliyebahatika kulala chali au walau mikono tu ndo kushka kitanda wakat miguu iko chini walitoka na majina yao tofauti,wengne walisema 'old traford' wengne 'darajani' na weng wao walipaita "MACHINJIONI" Geof hakuwa na kumbukumbu ya kulalamikiwa na msichana eti kuwa hajaridhika badala yake weng walimwambia "Geof unaniua" wakati kiuno bado wanazungusha.ah! mapenzi bwana.
# # # #
Sio waarabu,wahnd,waafrika ndo usiseme,hao wote Geof aliwatumia ipasavyo,na waliridhka wote,hakuna marefu yasiyokuwa ncha,Geof hatimaye alimaliza shahada yake ya elimu katika chuo kikuu cha dodoma "Go East go West home is the best" Geof akarejea kwao Tanga kupumzika na kuingia rasmi katika vita ya kutafuta ajira njema na kusaidia familia yake iliyokuwa duni sana baada ya mzazi wa kiume(Kazimoto) kuwa ametangulia kwenye haki mapema.Shule za serikali ni jambo ambalo Geof hakutaka kulisikia kwa sababu ya malipo duni sana
Miezi miwili ilikatika mambo yakiwa bado hayaeleweki,lakin Mungu si Athuman,mwanzon mwa mwez wa tisa ikiwa ni mitatu tangu amalize chuo alipokea barua kutoka shule ya sekondar Chacha Wangwe iliyojengwa na aliyekuwa ma jimbo la Tarime mkoani Mara,"Mh! mama huko siend"Geof alimwambia mama yake ambaye pia hakupenda mwanae mpenz aende huko kwa sababu ya iman potofu juu ya ukatili wa watu wa mkoa wa Mara hasahasa Wakurya"Mwanangu nenda ukajaribu ni Mungu amepanga huwezi jua" maneno meng ya mama yalimwingia Geof japo kwa shngo upande akakubali kwenda.safari iliandaliwa haraka ili Geof aendane na ratiba ya shule aliyoamua kwenda kufanya kazi "Mwanangu jiepushe na vibinti vitakuharibia kaz yako,kumbuka sana kumwomba Mungu,baba yako angekuwa hai angefurah kuona unaenda kazin kwa mara ya kwanza,alale pema 
 Kadri basi la Sumry lilivyozidi kuiacha ardhi ya jiji kivuli la Tanga (Mniwie radh watu wa tanga) na kuitafuta kwa kasi ardh ya jiji maarufu la Dar-es-salaam,ndivyo taratibu Geof aliyekuwa ameketi siti moja na mama mjamzito alianza kupitiwa na usingizi,sijui ni kwa sababu aliwah kuamuka au ni kukosa la kuongea na mama yule wala mtoto aliyeko tumboni mwake,safari yake ya usingizi ilikatishwa na kichwa cha yule mama kwenye mapaja yake "He! huyu mama ni usingz au ana nitafuta mengne mtoto wa watu mie" alijisemea Geof huku akimwangalia yule mama anavyokoroma kwenye mapaja yake.Kwa upole geof alimshtua yule mama "Samahan mwanangu jana sikulala kabisa" yule mama katumbo aliomba radh baada ya kugundua alikuwa amemlalia geof kimakosa.
Majira ya saa nne asubuh tairi za basi la sumry zilikuwa zinapapasa stend ya ubungo tayari kwa safar nyingne mchana huo.

*...,...*........*.....*......*...
Marry Mwita Wambura,binti halisi wa kikurya kuanzia sura hadi tabia,aliyajua maisha magumu ya kukata kuni,kukamua n'gombe,kuchunga mifugo na kupika ugali mkubwa mwekundu kwa ajili ya wanaume katika familia kubwa ya Mzee Mwita,aliyaish maisha hayo kwa miaka 19 ya usichana wake katika vijiji vitatu tofauti,alizaliwa miaka 23 iliyopita katika kijiji cha matare wilayani Mugumu Serengeti,baada ya miaka mitatu akaenda kuish kwa shangazi yake kijijini Nyarukongo wilaya hyo hyo.Had anafikisha miaka kumi na tatu na kutolewa bikra yake na baiskel bila kujitambua bado Mary alikuwa mtu wa vijijin had pale alipopata fursa nyingne ya kwenda kulea mtoto kwa shangazi yake musoma,kwake yeye ilikuwa zaid ya safari alipata wasaa wa kuona barabara ya lam kwa mara ya kwanza,magari meng na umeme ambao alikuwa anausikia tu,kijiji cha Nyamatare mjin musoma ndio Mary alifikia.Kwake kila siku ilikuwa furaha na furaha ilizid baada ya kupewa taarifa kuwa shangazi yake wa dar es salaam atakuja kumchukua siku moja,kwa habar alizosikia pale musoma kuhusu uzuri wa jiji hilo alitaman sana hyo siku ifike.Hakujua chungu tamu ya jiji la dar alichowaza yeye ni furaha(Nani ambae alikasirika alipoambiwa safari ya kuja dar kwa mara ya kwanza?)

##### ############# ######

Kichwa cha kuku kamwe hakibeb mzigo gari la Super Najimunisa alilopanda Geof lilipokuwa linaipita dodoma kumbukumbu nzuri ya kitanda cha sita kwa sita ilimrejea Geof kwa kas kubwa,kutahamak surual yake nyepes ilikuwa imeanza kunyanyuka maeneo husika."Dah! watanikoma hao wanaojiita sijui Wakula au Wakurya nitawageuza Wakuliwa" alijisemea geof kisha akatoa tabasam hafifu huku akirekebisha vurugu zilizotokea chn ya suruali.maneno aliyoshaur mama yalikuwa yamefifia kwenye akil ya geof."Sijui na huko watanipa sita kwa sita!" alijiuliza kisha akajipa jibu "Hata wakinipa mkeka mi mkali popote,nimekubalika dodoma ije kuwa huku?"
Sandra Maron,au maarufu zaidi kwa jina MAMAZ jijin Dar-es-salaam umaarufu wake ulitokana na pesa na samani nying alizokuwa anamiliki,inasemekana albino wana ngozi moja lakini kwa mama huyu mnene mfupi na mwenye pua kubwa iliyoenda sambamba na mdomo mpana uliopanuka muda wowote na kutoa matusi,kwa mtazamo wa haraka haraka zamani alikuwa ni kati ya wasichana waliotongoza wanaume kwani laiti angesubiri mwanaume amtongoze ingemgharimu kujitegesha kilabuni wanaume walewe gongo ndio kwa bahati mbaya wangeweza kujikita katika himaya yake,mamaz alikuwa hana mvuto kabisa machoni pa mwanaume yeyote aliye timamu kichwani.Ni mamaz huyohuyo katika jiji hili la Dar es salaam alikuwa ni kati ya wanawake waliokuwa wana soko kubwa kwa wanaume nadhani kwa sababu ya pesa zake na wala si lolote jambo kwa sababu kama ni mvuto hakuwa nao hata kiduchu.Ngozi yake ilikuwa imechubuliwa kuanzia usoni hadi kwenye unyayo wa miguu,hakuwah kutembea kwa miguu umbali zaidi ya mita kumi na tano,jeuri ya pesa ilimtawala.
Maduka yake makubwa mawili ya kuuza simu mtaa wa congo na uhuru pamoja na hoteli ya kawaida tu ya Mamaz maeneo ya Buguruni havikutosha wala havikufanana na utajiri mkubwa wa mama huyu wa kikurya ambae alipakataa kwao miaka ming iliyopita,alipoingia dar es salaam alikuwa anaitwa Sandra Marwa,lakini kwa kipindi cha hv karibuni kama ulitaman kulala kituo cha polisi kwa wiki moja bila kujua kosa lako thubutu kusema Mamaz ni mkurya,au mtanzania wa kuzaliwa,alichokibadili na kutaka kiwe hvyo ni kwamba yeye ni msomali baba yake ni wa huko na mama ni mwarabu.ha ha ha! huyo ndio Sandra Maron (Marwa) mh! natamani baba yake angefufuka mara moja amwone mwanae mpenzi.
Jasiri aach asili,baada ya miaka ming kupita na Mamaz alipokumbuka kuwa siku akifa atarud kuzikwa kwao basi akaamua kufunga safari kwenda kujenga nyumbani kwao tarime,msafara wa magari matano ya kifahari pamoja na fuso iliyoshehen vifaa vya ujenzi uliwasili Tarime mjin majira ya saa tatu asubuh kutokea Mwanza walipolala jana yake..

### ### #### ######
Gari la kampuni ya usafirishaji ya Bunda bus ndio ilimfikisha Geof Tarime ambapo alipokelewa na makamu mkuu wa shule moja kwa moja akapelekwa shulen kwa ajili ya kusaini mkataba na kuwa mwajiriwa rasmi."He? hawa watoto?,wanawake au mabinti" Geof alikuwa akijiuliza,kichwa chake kikiwa kimegeuziwa nje ya dirisha akitazama jinsi watoto wa kike walivyokuwa na vifua vikubwa "Du? au wana tenda ya kunyonyesha?" alijiuliza lakin hakuwepo wa kumjibu,alitaman kumuuliza yule dreva lakin akahofia jibu atakalopewa."He! yule anayeendesha ile baiskel mwanaume au mwanamke?" lilikuwa swal jingne gumu lakin hili jibu lake lilikuwa wazi sana alikuwa mwanamke ananyonga baiskel yenye gunia mbili ya mkaa huku mgongon akiwa na mtoto."Hawa ndo wakurya hutaki andamana".Zoezi la kusain mikataba halikuchukua muda mrefu,Geof baada ya zoezi hlo alichukuuliwa tena na kupelekwa Guest na kuhaidiwa kuwa atakaa pale kwa siku tano wakati nyumba atakayoish ikiendelea kuandaliwa "Sijui niwaambie kuhusu kitanda?" alijiuliza tena Geof lakin kabla hajauliza tayari gari lilikuwa linaunguruma kuashiria kuondoka."GIMANCHE GUEST HOUSE" ndio jina lililowapokea kina Geof.chumba namba 5 ndio ilikuwa halali ya Geof,"Karibu kaka" sauti nyororo lakin yenye mikwaruzo ilimkaribisha huku mkon uliokomaa ukifungua mlango wa chumba "Yes?!" Geof alijikuta akiruka juu kwa furaha na kumwacha yule muhudumu mdmomo wazi.
 "Vp kaka mbona umefurah hvyo? tena ghafla tu" aliuliza yule dada huku akimshangaa Geof."Mh! aah! unajua leo n4 birthday yangu." alijibu geof lakini yule dada hakuonyesha kumuelewa vizuri.Taratibu alisukuma mlango akamkaribisha ndani Geof tena."Utatumia chakula gani?" aliulizwa geof huku akiendelea kukitathmin chumba kwa macho yake,"Chochote tu dada" "Chochote? we nikikuletea kichuri utakiweza kweli" aliuliza yule dada (Kichuri ni kinyesi cha mbuzi kinachokutwa kwenye utumbo mwembamba wa mbuzi akichinjwa,huwa kwenye mfumo wa majimaji) "Kichuri ndio nini?,ah! hata hvyo mimi huwa sichagui chakula ntakula tu" alijiuliza na kujipa jibu mwenyewe."Haya kaka badae" aliaga binti yule mwenye lafudh ya kikurya ambapo hakujua wapi pa kuweka "LA" na wapi kuweka "RA".
Chumba kilikuwa self-contained,Geof alijifunga taulo yake akaingia bafuni kujisafisha mwili,baada ya hapo alirejea kitandani akajilaza akitafakari mambo mbalimbali lakini kubwa zaidi likiwa ngono Geof alijiona amemis sana kamchezo hako na kitanda alichokuwa amelalia ndio kilimletea hisia kali zaidi "Mh! nitaua wakurya wa hapa kwa huu ugwadu!" alijisemea geof kabla ya kukatishwa na hodi mlangoni,"Aah? vp ulikuwa bafuni?" Geof na yule binti walijikuta wanaulizana pamoja kutokana na mavazi waliyokuwa wamevaa,Geof kifua waz na taulo kiunoni,wakati yule bint alikuwa amevaa 'under-skirt' ya njano na juu amejitanda kitenge "Mh! mara yangu ya mwisho kuona haya manguo sjui ni lini"Alijiuliza geof."Mi nilikuwa najiandaa kulala vp wewe?" "Mi nimetoka kuoga sasa hv"Alijibu geof huku akipokea kile chakula na wote wakawa wanacheka chni chni."Kumbe unalala hapa hapa? hv unaitwa nan vile!" geof alimuhoji yule binti alivyoaga anaondoka "Naitwa Wegesa,nalala hapa hapa" "Mh! hauogopi kumbe" "Nimezoea" "Jina lako limekufanana yani zuri kama wewe" alidanganya geof huenda alimaanisha kinyume chake "Umetokea wapi mwalimu" "Nimetoka dar,naitwa geofrey" "Weweee umetoka dar? jamani pazur sana napapenda sijui nitaenda lin" Wegesa alionyesha dhahiri ameshangaa.mshangao wake ulizidi baada ya simu ya geof iliyokuwa ndan ya surual yake pale kitandan kuita mlio wa wimbo wa Marlow bembeleza,"Jamani had Alikiba na Mpenzi jini ipo"Alihoji kwa shauku huku akikaa karibu kabisa na geof "Kila kitu kimo hadi profesa jay,unamjua huyo"Geof alimjibu huku akisikilizia joto la Wegesa linavyopenya taulo yake,taratibu jogoo akaanza kunyanyuka "Leo ukipona mimi sio Geofrey" alijisemea huku akimgusa Wegesa mikono yake wakati anamwelekeza jinsi ya kutafuta nyimbo

#### #### ### ###
Mamaz alidhania suala la kusimamia ujenzi ni dogo sana kwake lakin ndan ya muda mfup alikuwa amechoka na kugundua kwamba alikuwa anakosa madili yake meng jijin dar-es-salaam.Hakuna jambo ambalo Mamaz hakulipenda kama mtu tofauti na yeye kusimamia kazi yake lakin kwa wakati huu ilimlazimu kusalimu amri,aliamua kumkabidh dada yake aliyekuwa anaish musoma kaz hiyo.
Akiwa na mpambe wake katika gari yake aina ya "VX" walitumia masaa mawili kuingia Musoma mjini,kwa mawasiliano ya simu walifanikiwa kumpata mwenyej wao mapema,walielekea moja kwa moja nyumbani kwake,hadh yao haikuwa ya kukaa pale kutokana na utajiri uliodhihirishwa na mavazi yao ya bei ghali."Marry! njoo umsalimie shangaz yako".....blauz yake nyepesi iliyokuwa imeloana kutokana na shughuli ya kufua aliyokuwa nayo iliruhusu chuchu zake zilizokuwa wima kabisa kuonekana,kanga moja iliyokuwa na chupi peke yake chn yake ilitoa uhuru kwa makalio yake kurukaruka kwa zamu "Nyakoromwita" "Nyamwita" walisalimia kwa kikurya."Shost hebu angalia hyo namba kama unaifahamu"Yule mpambe alimwambia Mamaz huku akimpa simu "Mh.shoga na huyu wamtaka tena kwa sababu hayo matamanio mh." haikuwa namba ulikuwa ni ujumbe wametumiana "ATATUFAA SANA" mamaz alijibu kwa ujumbe pia.
"Mh! huwa sipendi mwanga wa taa mimi,yani huwa napenda mwanga wa simu unanitosha kabisa yaan" Geof alimzuga Wegesa naye akiwa bize anashangaa simu akajikuta akisema bila kuangalia mbele "Swich ile pale mlangoni zima tu" harakaharaka Geof akawa tayari ukutani akabonyeza swich ukabakia mwanga wa simu peke yake pale chumbani "Ulisema unalala peke yako kule chumbani eti Wegesa" Geof aliuliza kinafiki kama vile amesahau kama jibu alikuwa amepewa tayari,hata hamu ya kula hakuwa nayo tena "Eeeh narara mwenyewe".Mwanaume ni mwanaume tu siku zote kwa janja ya panya kutawala paka akizubaa Geof aliufunga mlango kwa funguo bila Wegesa kusikia kutokana na mawazo yake yote kuwa kwenye simu,kisha akauficha kwenye 'boxer' yake aliyokuwa amevua wakati anaenda kuoga."Wegesa mi ngoja nijilaze kidogo nikiamka nitakula" "Haya...." alijibiwa.Geof hakuwa na wasiwasi ni kweli alilala akijua fika lazima Wegesa akitaka kuondoka lazima atamwamsha amfungulie.
"We kaka,we kaka,kaka jamani" ilikuwa ni sauti pekee iliyokuwa inatawala chumba cha Geof,ukimwa ulikuwa wa hali ya juu sana,yalikuwa majira ya saa saba usiku na kama dakika tano hv."Mhh! nani nini una....mh!" sauti ya ulev wa usingizi ilimjibu Wegesa "Mh! we unalala wewe,yani nimeiita" "Unasemaje simu mbona umezima?". Geof aliuliza "Hamna ni yenyewe imezima" alijitetea Wegesa.Geof kwa kujifanya hajui kama mbele yake kuna binti alipapasa na kukutana na kifua cha Wege,matarajio yake eti labda atashtuka ilikuwa kinyume alisogea tu pembeni."Nifungulie nikarare" aliomba wegesa."Mh? funguo zipo hapo mlangoni" "Hazipo bana" "He! hebu washa taa hapo" alisema Geof "Umeme umekatika,sijui ni luku imeisha" "NINI umesema umeme umefanyaje?" Geof alishtuka sio kwa mshangao bali kwa furaha tena furaha kubwa

* * * * *

Pesa zote na utajiri aliokuwa nao Mamaz haukuwa mwepesi kama ulivyotazamwa na wengi waliodhan ni maduka aliyokuwa nayo ndio chanzo,walisahau kujiuliza yalipatikana vp yale maduka.
Mamaz akiwa binti wa miaka 15,alipelekwa na rafiki yake nchini Kenya ambapo alitumbukizwa katika biashara chafu ya ukahaba ambayo alibobea na hatimaye alipofikisha miaka 20 alianza kuigiza mikanda ya ngono nchini Uganda kazi aliyoifanya kwa mafanikio makubwa sana kwa miaka mitano malipo yalikuwa mazuri sana hasahasa walipofanya na watu kutoka ulaya na Asia,kwa kipind hcho chote Mamaz alikuwa anahfadh pesa kwa wing na lengo lake likiwa kuukimbia umaskin kwa hali yoyote ile "Sitaki kuwa maskin" ni usemi huo uliompelekea yeye(Mamaz) kumshawish rafiki yake aliyemtoa Tarime na kumpeleka Kenya badae Uganda kuwa waanzishe kampun yao binafsi,katika nch jiran ya TANZANIA.




Nin kitaendelea!

"AGAINST WOMEN"

"AGAINST WOMEN"

Simulizi ya Against Women nimeiachia rasmi check my Notes facebook kujipatia uhondo.

Saturday, November 6, 2010

"AGAINST WOMEN-introduction"

Christian ni kijana mtanashati aliyelelewa katika kituo cha watoto yatima baada ya mama yake kumtelekeza,kadri anavyozid kukua anapata wito wa kuihubiri injili na kueneza amani na upendo duniani,akiwa na miaka 16 anatolewa pale kituoni kwa ahadi ya kwenda kusomea masomo ya upadri lakini mwanamama mmiliki wa kituo hcho anamgeuza mtoto huyo kama muhudumu wake kimapenzi,Christian anaish katika kifungo hcho kwa miaka mitano,alipofanikiwa kutoka hapo anabadilika na kuwa mtu tofauti kabisa na kuitikisa Nchi nzima

*Chris alitoka vp katika kifungo.
*Ni hatari ipi anayokuja nayo Chris.
*Huyo mwanamama ni nani?

TWENDE PAMOJA KATIKA BLOG HII.

"AGAINST WOMEN-01"